February 10, 2016

MANJI
Kikosi cha Yanga sasa kinaondoka Ijumaa kwenda nchini Mauritius kwa ajili ya mechi yake ya Ligi ya Mabingwa.

Awali, uongozi wa Yanga, jana uliwatangazia waandishi wa habari kwamba Yanga itaondoka leo alfajiri.

Taarifa zinaeleza kwamba, Manji ameamua kuikodia Yanga ndenge maalum baada ya kupata taariafa kungekuwa na suala la wachezaji wa Yanga kukaa uwanja wa ndege kwa saa saba na pia wakati wa kurudi wangelezimika kulala Johannesburg.


Lakini Msemaji wa Yanga, Jerry Muro amesema kwamba kamati ya mashindano imeshauriana na uongozi na kuona ni muhimu timu ikiondoka Ijumaa.

“Nisingependa kuzungumzia suala la nani kakodi ndege, wewe jua Yanga sasa itaondoka Ijumaa badala ya leo kwa sababu hizo za kiufundi.


“Uongozi na kamati ya ufundi imeona ni bora wachezaji waondoke Ijumaa kwa ajili ya kupunguza uchovu. Kama wangeondoka leo, saa saba pale uwanja wa ndege lisingekuwa jambo zuri kwa afya ya mchezaji.

“Angalia, wangeondoka alfajiri, wangefika Afrika Kusini saa mbili na nusu hivi. Halafu wangeendelea kuwa uwanja wa ndege hadi saa nane mchana kusubiri ndege ya kwenda Mauritius.

“Hivyo Ijumaa  ndiyo siku sahihi, tutatumia saa nne tu hadi Mauritius na baada ya hapo ndege itakuwa ikitusubiri na tutageuza nayo,” alisema Muro.




0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic