February 14, 2016


Mshambuliaji Mtanzania, Mbwana Samatta ameichezea timu yake ya KRC Genk kwa mara ya pili katika mechi ya Ligi Kuu Ubelgiji.

Samatta anayevaa jezi namba 77 aliingia katika dakika ya 77 wakati Genk ikiivaa Waasland na kuichapa kwa mabao 6-1.

Alichukua nafasi ya Nikos Karelis aliyekuwa amefunga mabao mawili kati ya sita ya Genk.

Hii ni mara ya pili kwa Samatta kuanzia benchi na kuingia. Hata hivyo kocha anaonekana kumuamini, kwani mechi ya kwanza amempa nafasi ya kukaa benchi na baadaye kuanza kama ilviyokuwa katika mechi ya pili.


Samatta amejiunga na Genk akitokea TP Mazembe ya DR Congo ambayo aliisaidia kubeba ubingwa wa Afrika.

1 COMMENTS:

  1. mmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmmhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhanajuaaaaaaaaaaaaaaaa kwan huyo

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic