April 6, 2016


Wakati Yanga ikishuka dimbani wikiendi hii kumenyana na Al Ahly katika mchezo wa Klabu Bingwa Afrika, beki na nahodha wa muda wa kikosi hicho, Mtogo, Vincent Bossou, ametamka kuwa yupo fiti kukabiliana na straika hatari wa wapinzani wao hao, Mgabon, Malick Evouna, ambaye ndiye mchezaji hatari kwa upande wa Waarabu hao.

Bossou anaweza kuwa sehemu ya kikosi cha kwanza cha Yanga kitakachoanza katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Al Ahly, mchezo utakaopigwa Uwanja wa Taifa Aprili 9, mwaka huu.

Bossou ambaye amewahi kucheza soka la kulipwa Vietnam amesema kuwa licha ya mashabiki mbalimbali kuwa na hofu na kiwango chake lakini yupo vizuri kuhakikisha anasaidia timu yake hiyo kupata ushindi.

“Sina hofu hata kidogo katika mchezo huo kutokana na maandalizi mazuri ambayo tunaendelea kujipa ikiwemo ya kuingia ‘gym’ kwa ajili ya kuongeza stamina na nguvu za kupambana kwani tunajua wachezaji tunaokutana nao wako fiti kiasi gani,” alisema.


Al Ahly walitarajiwa kuingia nchini usiku wa kuamkia leo kwa ajili ya mchezo huo ambao marudio yake yanatarajiwa kuwa ni kati ya Aprili 19 mpaka 20, mwaka huu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic