April 30, 2016


MPIRA UMEKWISHAAAA
-Mashabiki wanaonekana kuanza kutoka nje ya uwanja, wengine wakizomea kipa wa Yanga kujilaza
-Dida analala chini akionekana kupoteza muda, anasema misuli imembana. DAKIKA 2+ ZA NYONGEZA
Dk 90, Kimanzi anapiga shuti lakini mpira unapita juu kidogo ya lango

Dk 89, Yanga wanatumia akili zaidi, wanacheza taratibu huku wakizuia mpira kwenda kwenye lango lao
SUB DK 88, Evarist Benard anaingia kuchukua nafasi ya Waziri Junior kwa upande wa Toto
Dk 87, Anthony anapiga shuti kali akiwa umbali wa takribani mita 27 hivi, linatoka nje kidogo ya lango la Yanga
Dk 86 krosi safi kabisa ya Kimanzi lakini inapi juu ya lango la Yanga
Dk 83 hadi 85, Yanga wanaonekana kumiliki mpira kupoteza muda, lakini Toto hawana presha kubwa kuwapokonya

Dk 82, Ngoma anaangushwa na taratibu anaibuka na Juma Abdul anauchonga mpira ule kwa shuti kimo cha paka lakini Toto wanaokoa
SUB Dk 79 Yanga inafanya mabadiliko kwa kuwatoa Kaseke, Tambwe, Niyonzima na kuwaingiza Matheo, Kamusoko na Busungu. Kocha Hans van der Pluijm ameamua kufanya sub ya watu watatu kwa mpigo

GOOOOOOO Dk 77 Juma Abdul anaifungia Yanga bao safi kwa shuti kali, ilikuwa ni baada ya kipa kuokoa mpira wa kurushwa wa Oscar Joshua, mabeki wakaokoa shuti la Msuva na Juma Abdul akatandika shuti kali kabisa

Dk 74, Matheo Anthony, Thabani Kamusoko na Malimi Busungu wanaonekana wakipasha misuri pale nje
Dk 72, Khatibu anafanya kazi yaz iada kuokoa mpira wa krosi wa Juma Abdul inakuwa kona, inachongwa na Kaseke lakini ni rahisi kabisa kwa kipa

Dk 65 hadi 69, mpira zaidi unachezwa katikati ya uwanja, hakuna mashambulizi makali
Dk 63, Kimanzi anamtoka Bossou hapa na yeye anamvuta na kumwangusha kwenye eneo la hatari lakini mwamuzi anasema ni kona inachongwa na kuokolewa kwa mkono na Dida
Dk 62, al manusura Ngoma afunge bao la pili la ,mpira wake unapita juu kidogo ya lango la Toto
KADI Dk 62 Carlos Protas anaonyeshwa kadi ya njano kutokana na kulalamika. Awali alilalamika na Tambwe akasawazisha

Dk 58 hadi 61, inaonekana mpira unachezwa katikati zaidi ingawa wachezaji wa Toto wanaonekana kuwa na hasira
Dk 57, kipa anatoka na kuokoa kwosi safi ya Joshua na Ngoma tayari alisharuka juu
DK 56 mwamuzi anawaita Tambwe na Mlipili na kuwaambia waache maneno na kucheza soka

Dk 55 sasa, timu zote bado zinacheza zikionekana kusaka mabao....lakini Toto African wanaonekana kutokuwa makini sasa katika safu ya ulinzi
GOOOOOO Dk 50, Tambwe anafunga bao safi kabisa kwa kichwa akiunganisha krosi nzuri ya Ngoma
Dk 47, Toto wanapoteza nafasi nzuri kabisa lakini Yondani anafanya kazi ya ziada kuokoa
Dk 46, Mpira unaanza, Yanga wakionekana kidogo kuanza kwa kasi lakini Toto pia wako makini kutibua kila mipango

MAPUMZIKO
-Kipa Mussa Mohammed anadaka mpira kwenye miguu ya Msuva aliyekuwa anajaribu kuuwahi
-Kidogo Yanga wanaonekana kuwa na papara na hofu kidogo
DAKIKA 2+ ZA NYONGEZA
Dk 42 hadi 44, Toto wanaonekana kuwa wajanja wakipoteza muda, huenda wanataka kwenda mapumziko wakiwa na bao hilo moja
Dk 40, kipa wa Toto yuko chini akidai ameumia, mwamuzi anaita waguzi
GOOOOOO Dk 39, William Kimanzi anakwenda kuandika bao la kwanza kwa Toto baada ya kuunganisha mpira wa kona uliochongwa na Kimanzi na kuandika bao kwa kichwa safi kabisa

Dk 37 kipa Dida wa Yanga anachochanya akiwa mwenyewe, anautoa mpira nje na kuwa kona
Dk 33, kipa Mussa Mohammed wa Toto anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa kichwa wa Tambwe. kaumia, yuko chini anatibiwa
Dk 30, Ngoma anamtoka beki mmoja wa Toto, anashangiliwa, anampa Niyonzima anapiga shuti kuuubwaaa, goal kick
Dk 29, Toto wanafanya mashala, nusura Ngoma aunase mpira lakini wanaokoa na kuwa kona, inachongwa na Msuva, ni kona dhaifu

Dk 27, kipa Toto shujaa tena, anaokoa mkwaju mkali wa krosi ya Msuva, Tambwe anaanguka baada ya kuukosa
Dk 23 hadi 25, Yanga ndiyo wanamiliki mpira zaidi, lakini bado mashambulizi ni mojamoja
Dk 22, Yanga wanapata kona nyingine, lakini kama zile za mwanzo, wanapiga na haina madhara hata kidogo kwa Toto...
Dk 20, Oscar Joshua anaachia shuti kali sana, lakini kipa Toto anaonyesha ubora na kupangua vizuri
Dk 19, Carlos Protus anafanya kazi ya ziada kuuwahi mpira ambao alipenyezewa Ngoma, anaotoa na kuwa kona. Inachongwa lakini haina madhara kwa Toto

Dk 14 hadi 18, mpira kidogo unachezwa zaidi katikati na hamu ya mashambulizi inapungua
inaonekana Dk 13, Ngoma na Msuva wanagongeana safi, Msuva anatoa pasi au krosi nzuri kabisa lakini Ngoma anaukosa mpira...
Dk 10, nafasi nzuri zaidi hadi sasa anaipata Waziri Junior akiwa peke yake, anaruka juu na kupiga mpira juuu ya lango la Toto

Dk 7, Msuva ainaingia na kupiga kona safi kabisa, lakini hakuna mtu, Toto wanaokoa, kona. Inachongwa vizuri lakini haina faida kwa Yanga

Dk 6, Niyonzima anapiga pasi nzuri kabisa katikati ya lango la Toto, mabeki Toto wanajichanganya wakidhani offside lakini hakuna mtu pale
Dk 3, Waziri Junior nusura autumbukize mpira wavuni lakini Yondani anaondosha
Dk 1 tu, Toto wanapata kona, anaichonga Seseme, inaokolewa na kuwa mpira wa kurushwa. Yanga wanaondoa sehemu ya lango lao
Mechi imeanza hapa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Toto African wakiwa wenyeji dhidi ya Yanga wanaowania ubingwa.


Kama Toto African watashinda leo watakuwa wamejihakikishia kubaki Ligi kuu Bara na Yanga wakishinda, watakuwa wamebakiza sehemu chache kujihakikishia kutwaa tena ubingwa.

1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic