April 15, 2016



SHAKHTAR DONETSK vs SEVILLA

VILLARREAL vs LIVERPOOL




Droo ya Nusu Fainali ya Uefa Europa League imefanyika na tayari timu nne zilizoingia katika hatua hiyo zimepangwa jinsi zitakavyokutana.


Villarreal imepangwa kuanza mechi ya kwanza ya hatua hiyo kwa kuikaribisha Liverpool wakati ambapo Shakhtar Donetsk itacheza dhidi ya Sevilla.


Nusu fainali ya kwanza inatarajiwa kuchezwa Aprili 28 wakati ambapo mechi za marudio za hatua hiyo zitachezwa Mei 5, 2016.



Fainali ya michuano hiyo inatarajiwa kuchezwa Mei 18, 2016 kwenye Uwanja wa St. Jakob-Park jijini Basel nchini Switzerland. 



Liverpool imetinga hatua hiyo baada ya kuitoa kimaajabu Borussia Dortmund ya Ujerumani katika Robo Fainali kwenye Uwanja wa Anfield kwa mabao 4-3 licha ya awali wapinzani wao hao kuongoza kwa mabao 2-0 kisha 3-1 lakini bado vijana wa Kocha Jurgen Klopp wakapambana na kupata ushindi huo.


Katika mechi ya kwanza baina ya timu hizo, matokeo yalikuwa 1-1, hivyo jumla Liverpool imesonga mbele kwa jumla ya mabao 5-4.



Villarreal imekuwa na mwendo mzuri katika Ligi Kuu ya Hispania ‘La Liga’ ambapo inashika nafasi ya nne, iliitoa Sparta Prague ya Czech katika Robo Fainali kwa kuifunga mabao 6-3.


Vijana wa Ukraine, Shakhtar Donetsk ambao waliwatoa Braga wa Ureno, wao wataanzia nyumbani kisha wiki moja badaye watawafuata wapinzani wao, Sevilla ambao walitinga hatua hiyo kwa kuwatoa Athletic Bilbao kwa mikwaju ya penalti.






0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic