May 2, 2016

NGASSA WAKATI AKIENDELEA NA MATIBABU BAADA YA UPASUAJI WA GOTI...
 Mshambuliaji nyota wa Free State Stars ya Afrika Kusini, Mrisho Ngassa ameanza mazoezi taratibu baada ya kuhangaika na maumivu kutokana na upasuaji wa goti aliofanyiwa.

kutoka nchini Afrika Kusini, Ngassa ameiambia SALEHJEMBE kwamba ameanza mazoezi kuhakikisha anajiweka fiti.

“Ni mazoezi ya taratibu sana. Naanzia gym halafu baada ya hapo ni uwanjani lakini taratibu,” alisema.

Ngassa amekaa takribani mwezi nje ya uwanja akiuguza maumivu hayo na baadaye alifanyiwa upasuaji huo ambao ulikwenda vizuri.

Kiungo huyo mwenye kasi kutoka jijini Mwanza, amesema ana imani kubwa mambo yataenda vizuri baada ya muda.

“Ni suala la subira tu, ninaamini baada ya muda mambo yataenda vizuri. Zaidi nimekuwa nikizingatia maelekezo,” alisema akionyesha utulivu.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic