HALL |
Kocha Stewart John Hall, sasa si kocha wa Azam FC tena.
Hall raia wa Uingereza amekaa meza moja na Azam FC, wamekubaliana na amebwaga manyanga, anaondoka zake.
Uongozi wa Azam FC, umethibitisha kwamba Hall si kocha wao tena baada ya kumalizana naye.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba, amesema: "Kikosi sasa kitabaki chini ya kocha msaidizi, Dennis Kitambi na ndiye atamalizana nayo ligi pamoja na mechi ya fainali ya Kombe la FA dhidi ya Yanga.
“Tumekaa pamoja na kukubaliana pande zote mbili, alituomba kuachia ngazi kwa lengo la kutafuta changamoto nyingine nje ya nchi.
“Tunamtakia kila la kheri aendako, pia tunamshukuru kwa mafanikio kwani tuko nafasi ya pili katika ligi na pia fainali ya Kombe la FA."
REKODI ZA HALL:
MECHI 62
SHINDA 41
SARE 16
POTEZA 5
Hii ni tokea alipotua Azam FC Juni, 2015.
MABAO YA KUFUNGA 111
MABAO YA KUFUNGWA 41
BILA KUFUNGWA (Mechi 31)
0 COMMENTS:
Post a Comment