June 24, 2016


Siku moja tu baada ya kuingia mkataba mpya na kampuni maarufu ya kuuza matairi nchini ya Bin Slum Tyres, klabu uya Mbeya City imeanza kuonyesha jeuri ya fedha.

Mbeya City imeingia mkataba na kiungo mshambuliaji kutoka Prisons ya Mbeya pia, mohammed Mkopi.

Mkopi amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuichezea Mbeya City ambayo imesaini mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya Sh milioni 300 kupitia bidhaa za betri za magari za RB kutoka kwa Bin Slum.

Awali, Mbeya City ilitaka kumchukua Didier Kavumbagu kutoka Azam FC, lakini raia huyo wa Burundi aliamua kwenda nchini Vietnam ambako ameanza maisha mapya ya soka.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic