June 26, 2016



Pamoja na kuendelea na usajili, klabu ya Simba imeweka nafasi kwa ajili ya kocha wake mpya ambaye kwa asilimia 95 atakuwa Joseph Omog.

Omog raia wa Cameroon aliyewahi kuipa ubingwa Azam FC, amekubaliana na Simba kila kitu na inaonekana ndiye atakuwa kocha mpya wa Simba kwa kuwa kocha Mghana, Tetteh anaonekana kutokuwa tayari kujiunga na Msimbazi.

“Unajua kocha anapokuja, lazima naye atakuwa na mawazo yake kuhusiana na suala la usajili.

“Pamoja na kufanya usajili, lakini kocha naye atawekewa nafasi kwa wachezaji wa kigeni pamoja na wale wa ndani,” kilieleza chanzo.

“Hii maana yake pamoja na usajili huo ambao ulifanywa na kamati ya ufundi na usajili, mwalimu naye anakuwa na nafasi ya kusajili pia.”


Simba inatarajia kuanza mazoezi rasmi kesho au keshokutwa kwa ajili ya kujiandaa na msimu mpya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic