July 4, 2016


Kipa namba moja wa Simba, Vincent Angban raia wa Ivory Coast, alishindwa kutua nchini usiku wa kuamkia jana kutokana na kuchelewa ndege alipokuwa akitokea nchini kwao.

Angban alitarajia kutua akiambatana na mshambuliaji mpya wa timu hiyo raia wa Ivory Coast, Blagnon Goue Fredric alishindwa kufanya hivyo huku Fredric ambaye alikuwa akiitumikia Klabu ya African Sports ya Ivory Coast akiwasili peke yake juzi usiku kisha akitarajiwa kufanya mazungumzo ya usajili kumalizana na uongozi wa Simba, jana Jumapili.

Habari za kuamnika kutoka ndani ya Simba zimedai kuwa kutokana na hali hiyo Angban anatarajia kutua nchini usiku wa kuamkia leo tayari kwa kuanza maandalizi yake kwa ajili ya msimu ujao.

“Mshambuliaji wetu mpya ambaye tunatarajia kumsajili hivi karibuni ambaye ni raia wa Ivory Coast tayari ameshatua na sasa yupo katika mazungumzo ya mwishomwisho na uongozi.

“Alikua aje na Angban ambaye alikwama kutokana na kuchelewa ndege, baada ya kuchelewa akaomba uongozi umuongezee fedha ile ambayo huwa inaongezwa inapotokea msafiri amechelewa ndege, uongozi ulikataa an ameongeza mwenyewe kwa kuwa ni uzembe wake,” kilisema chanzo kutoka Simba.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic