July 4, 2016


Kocha Mganda, Jackson Mayanja aliyeelezwa kuwa mbioni kuachana na Simba kutokana na sababu mbalimbali, ametua jijini Dar, juzi usiku na kufunguka kuhusiana na kocha mkuu mpya wa timu hiyo, Joseph Omog.

Mayanja ambaye ametua nchini akitokea Uganda alikokwenda kwa ajili ya mapumziko mara baada ya kumalizika kwa ligi msimu uliopita, hivi karibuni kuliibuka taarifa zilizodai kuwa hayupo tayari kufanya kazi chini ya Omog lakini amekanusha hilo.

“Kama nikielewana na Simba nitafanya kazi tu chini ya Omog kwa kuwa nafahamu majukumu yangu kama kocha msaidizi,” alisema Mayanja.

Awali kulikuwa na taarifa kuwa Mayanja anaweza kutua katika timu yake ya zamani ya Kagera Sugar au Mwadui FC, ambapo yeye mwenyewe amekiri kufanya mazungumzo na klabu hizo kwa kuwa mkataba wake na Simba ulimalizika.

“Kweli Kagera na Mwadui wananihitaji, hata Kiyovu SC ya Rwanda pia lakini nipo Dar kwa kuwa nimetumiwa tiketi na Simba. Hivyo, nitawasikiliza Simba kwanza baada ya hapo ndiyo kitakachofuata,” alisema kocha huyo.

Taarifa za ndani ya Simba zinaeleza kuwa Mayanja alitarajiwa kukutana na Omog, jana kwa ajili ya mazungumzo.


Akiwa kocha wa muda wa Simba, Mayanja aliiongoza Simba katika mechi 16 za Ligi Kuu Bara na kushinda 11, sare moja na kupoteza nne dhidi ya Yanga, Mwadui, Toto African na JKT Ruvu.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic