August 19, 2016



Straika nyota wa Yanga, Mrundi, Amissi Tambwe, ameamua kuweka wazi sababu za kukabiliwa na ukame wa mabao hasa katika michuano ya kimataifa kuwa kikubwa ni kubadilishiwa majukumu uwanjani.

Tambwe, mfungaji bora wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita, amesema kuwa zamani alikuwa akichezeshwa kama mshambuliaji wa kati namba tisa lakini kwa siku za hivi karibuni amekuwa akipangwa kucheza namba 10 akiwa nyuma ya straika, hali inayomfanya kuwa mbali na lango.

“Ni kweli mimi mwenyewe najiona nimepunguza kasi ya kufunga, nafikiri sababu kubwa ni mabadiliko hayo ya nafasi uwanjani, namba kumi inaniweka mbali na lango, hiyo inatokana na mfumo wa kocha tunaotumia kwa sasa.

“Kwa nafasi hiyo siwezi kufunga sana, japokuwa nitajitahidi kufanya hivyo lakini haitakuwa kama awali, ndiyo maana hata sasa hivi sionekani sana kwenye boksi la timu pinzani, kwa hiyo hata msimu ujao itategemea na kocha atakavyonitumia.

“Siwezi kupinga chochote kulingana na maagizo hayo ya kocha kwa kuwa yeye ndiye anayetambua umuhimu wangu na anaendelea kunipanga anapoona ni sahihi, mimi nitaendelea kutekeleza majukumu ninayopewa kama kawaida,” alisema Tambwe.

Kocha wa Yanga, Hans van Der Pluijm, amekuwa akimkabidhi majukumu ya namba tisa, Mzimbabwe, Donald Ngoma au Obrey Chirwa tofauti na awali ambapo hao walikuwa wakicheza nyuma ya Tambwe au pembeni.

SOURCE: CHAMPIONI.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic