September 16, 2016

Wakati kesho Jumamosi straika wa Simba, Mrundi, Laudit Mavugo akitarajia kuiongoza safu ya ushambuliaji ya Simba kuwavaa Azam FC, mshambuliaji huyo ameweka bayana alichokutana nacho kwenye mechi nne za Ligi Kuu Bara mpaka sasa.

Mavugo aliyeifungia Simba mabao matatu kwenye mechi nne, ametamka kwamba ushindani wa ligi hiyo ni mkubwa zaidi ya aliokuwa anakutana nao nchini kwao Burundi, ambapo mabeki wengi wamekuwa wakicheza zaidi ya kazi ili kulinda timu yao isifungwe.



Straika huyo wa zamani wa Vital’O ya Burundi ameliambia Championi Ijumaa, kwamba wapinzani wao hasa mabeki, wamekuwa wakiwafanyia vitendo visivyo vya kimichezo ili kuwaondoa katika hali ya kimchezo na pia wasipate nafasi ya kufunga mabao.

“Bongo mambo ni magumu kwa sababu wapinzani mara nyingi wanatufanyia vitendo ambavyo ni vya kukera na visivyo vya kimpira kwa lengo tu watuondoe katika hali ya kiuchezaji lakini pia hiyo ikiwa ni mbinu ya wao kujilinda.

“Lakini kwangu wala sijali na badala yake nitaendelea kupambana zaidi na zaidi kuitetea timu yangu kuhakikisha inaibuka na ushindi katika kila pambano,” alisema Mavugo.

SOURCE: CHAMPIONI

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic