September 11, 2016

Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi ameshitushwa na taarifa za tukio la tetemeko kubwa ardhi lenye mtikisiko wa kipimo cha Ritcher 5.7 lililotokea jana Septemba 10, 2016 katika mikoa mitatu ya Kanda ya Ziwa kadhalika nchi za Burundi na Uganda.

Mikoa ya Kanda ya Ziwa iliyopata athari kwa mujibu wa taarifa ni Mwanza, Mara na Kagera nchini na kuripotiwa kuua zaidi ya watu 10 na wengine zaidi ya 120 kujeruhiwa sambamba na kubomoa majengo mbalimbali.
 

Rais Malinzi mara moja anaungana na Serikali katika kusubiri tathmini na kisha kuangalia namna TFF itakavyoweza kusaidia kama sehemu ya wadau katika jamii. TFF inaamini kuwa baadhi ya waliopata maafa ni familia ya mpira wa miguu si ndani tu ya nchi, bali pia nje ya mipaka ya Tanzania.











Hivyo, Rais Malinzi ametutuma salamu za rambirambi kwa familia zote zilizopoteza ndugu, jamaa na marafiki na anawaombea marehemu wapumzishwe mahali pema peponi. Amina. Na amewaombea kwa Mwenyezi Mungu awape moyo wa subira na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Katika salamu hizo, pia Rais Malinzi amemtumia Rais Shirikisho la Mpira wa Miguu Burundi (BFF), Marlon Kuylen kwa sababu sehemu ya Bujumbura imeguswa na tetemeko hilo kadhalika ametuma salamu za rambirambi kwa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Uganda (FUFA), Moses Magogo baada ya ripoti kuonesha kuwa tetemeko hilo limeukumba mji wa Kampala na Rakai nchini Uganda. Wataalamu wa elimu ya miamba – Jiolojia wanasema kwamba lilikuwa ni kubwa kwa mujibu wa vipimo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic