September 27, 2016


Kocha Sam Allardyce ameachia ngazi ya kukinoa kikosi cha timu ya taifa ya England.

Allardyce maarufu kama Big Sam amedumu kwa siku 67 baada ya kupata mkataba mnono wa kuinoa England ambao thamani yake ulikuwa pauni milioni 3.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 61, ameingia kwenye mtego na kurekodiwa akipiga dili ya upindishaji wa sheria za FA.


Katika dili hiyo, Big Sam angefanikiwa kupata pauni 400,000 lakini alitegewa kamera ambayo picha zake zilisambazwa akijiachia, jambo ambalo limemfanya mwenye akubali kuachia ngazi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic