September 3, 2016



Baada ya kusubiri sana, hatimaye mshambuliaji mpya wa Yanga, Mzambia, Obrey Chirwa, jana alitoa ‘gundu’ baada ya kufunga bao lake la kwanza tangu atue kuichezea timu hiyo kwenye ushindi wa mabao 2-0.

Chirwa alifunga bao hilo wakati Yanga ilipocheza na timu yao ya vijana chini ya miaka 20 yaani U20 inayofundishwa na beki na nahodha wa zamani wa timu hiyo, Shadrack Nsajigwa.

Mzambia huyo, aliyetua kuichezea Yanga kwa dau la Sh milioni 200, amecheza mechi za Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya TP Mazembe, Medeama na MO Bejaia na nyingine ya kirafiki dhidi ya Mtibwa Sugar bila kufunga bao lolote.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Viwanja vya Gymkhana, Dar, mshambuliaji huyo, alifunga bao hilo katika dakika ya 17 akiunganisha krosi nzuri ya Thabani Kamusoko.

Chirwa amefunga bao hilo, akiwa ametoka kwenye majeraha ya goti aliyoyapata kwenye mechi dhidi ya MO Bejaia na amerejea uwanjani juzi Jumatatu.

Katika mechi hiyo, licha ya timu ya vijana kujitutumua kutaka kusawazisha bao hilo, Mzimbabwe Donald Ngoma aliifungia Yanga bao la pili kwa kumchambua kipa akipokea pasi ya Anthony Matheo.


Kikosi cha Yanga kiliundwa na Beno Kakolanya, Hassan Kessy, Oscar Joshua, Juma Makapu, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kamusoko, Matheo, Malimi Busungu, Chirwa, Ngoma na Yusuph Mhilu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic