October 7, 2016


Timu 12 zinatarajiwa kushiriki Ligi ya Taifa ya Wanawake inayotarajiwa kuanza Novemba mosi, mwaka huu kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Maendeleo ya Soka la Wanawake na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), zilizoridhia tarehe hiyo.

Tayari klabu zimeagizwa kuzingatia jina kuenenda na namba za jezi mgongoni ili kuepusha mkanganyiko wa wachezaji wakati wa ligi hiyo inayofanyika kwa mara ya kwanza nchini Tanzania.

Timu 12 zinatarajiwa kushiriki ligi hiyo ambako kesho Oktoba 8, 2016 itakuwa ni siku ya kuchambua fomu za usajili wakati Oktoba 10, mwaka huu majina ya usajili yatatangazwa ambako pia klabu zitatumiwa kupitia anwani za barua pepe.

Oktoba 11 na 12, 2016 ni muda wa klabu kuleta mapingamizi yatakayosikilizwa Oktoba 15, mwaka huu. Majina ya pingamizi yatatangazwa kabla ya Oktoba 20, 2016 na maandalizi ya ligi yataendelea.

Wakati wote huo wa usajili, klabu hazina budi kutangaza aina ya rangi wanazotumia katika michezo ya nyumbani na ugenini na kutakiwa kusafiri na jozi zote mbili ili kuepuka mkanganyiko wa kufanana jezi.

Kutakuwa na jopo la makocha watakaofanya uteuzi wa wachezaji nyota watakaoitwa kwenye timu za taifa ambaye atagharamiwa na TFF.

Vyama vya mikoa visadie klabu katika bajeti zao kwa vile tathamini inaonyesha kuwa fedha zinazotoka hazitoshi. Vyama hivyo vya mikoa pia visaidie maandalizi ya michezo kama vile kuandaa uwanja nakadhalika ukioandoa waamuzi ambao watagharamiwa na TFF.

Hakutakuwa na zawadi ya fedha zaidi ya kombe la medali kwa timu shiriki, labda kama atatokea mdhamini mwingine. Hakutakuwa na zawadi kwa mchezaji bora, mfungaji bora, kipa bora, ingawa kutakuwa na jopo la kuwachagua. Mchezaji bora atachaguliwa kwenye hatua za mwisho wa mashindano, mfungaji bora atachaguliwa kuanzia hatua ya kwanza ya mashindano.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic