November 30, 2016

AWADHI JUMA

Uliisikia hii taarifa? Imeelezwa kuwa kigogo mmoja wa klabu ya Simba, jina kapuni amezuia uhamisho wa mchezaji Awadhi Juma ambaye alitakiwa kupelekwa kwa mkopo katika timu ya Kagera Sugar katika usajili huu wa dirisha dogo kwa madai ya kiwango chake kushuka.

Awadhi ni miongoni mwa wachezaji kadhaa wa Simba ambao hawakupata nafasi ya kucheza mechi hata moja katika mzunguko wa kwanza wa ligi kuu kutokana na kocha Joseph Omog kutompanga katika kikosi chake.

Chanzo kutoka Simba ambacho hakikutaka kuweka wazi jina lake kimeeleza kuwa, kuna baadhi ya viongozi walikuwa katika mipango ya kumtoa kwa mkopo kiraka huyo kwenda Kagera Sugar lakini jaribio lililogonga mwamba.

DEWJI (KULIA) AKIWA NA HASSAN DALALI

“Awadhi ni miongoni mwa wachezaji ambao walikuwa kwenye mipango ya kutolewa kwa mkopo katika usajili wa dirisha dogo kutokana na kutopata nafasi ya kucheza mzunguko wa kwanza.

“Maamuzi hayo yalipingwa vikali na kigogo mmoja wa Simba kufuatia kuutambua vilivyo uwezo wake kutokana na kuwa mchezaji muhimu katika timu hiyo, lakini pia ni kwa kuwa anaweza kucheza namba nyingi uwanjani,” kilisema chanzo hicho.

SOURCE: CHAMPIONI





0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic