November 6, 2016


Kocha Joseph Omog ameonyesha alivyo bora katika suala la saikolojia baada ya kuwaambia wachezaji wake, kazi haijaisha.

Omog raia wa Cameroon, amesema waliweka nguvu kubwa kwa Stand United kwa kuwa walijua ni timu ambayo haijapoteza mchezo kwenye Uwanja wa Kambarage na tayari iliisha vifunga vigogo, Yanga na Azam FC.

“Kasema baada ya hapo, African Lyon ni timu nyingine ngumu. Wachezaji hatupaswi kufikiria kazi imeisha.

“Ule mwendo ambao tumekuwa tukienda nao au tulioutumia dhidi ya Stand, dhidi ya Lyon inabidi iwe zaidi,” alisema mmoja wa wachezaji wa Simba.

Simba ndiyo vinara wa Ligi Kuu Bara na hawajapoteza mchezo hata mmoja kati ya 13 ambayo wamecheza.


Leo wako Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam kucheza mechi yao ya 14.

Katika saikolojia inaonyesha, kila binadamu baada ya kazi nzito hupenda kupumzika. Omog amejua wachezaji wake wangefurahi kupumzika au kuona kazi imeisha baada ya mechi ya Stand, jambo ambalo ni hatari kwao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic