November 4, 2016


Beki wa Yanga, Vincent Bossou, ametamka hadharani licha ya kukubali kipigo cha mabai 2-1 kutoka kwa Mbeya City lakini hatamsahau mwamuzi wa kati wa mchezo huo, Rajab Mrope kutokana na maamuzi yake kuwa tata.

Yanga ilipata kipigo hicho kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya katika mchezo wa Ligi Kuu Bara, juzi, ambapo beki huyo raia wa Togo anasema hajawahi kuona maamuzi kadhaa yaliyofanywa na refa huyo.

“Tumefungwa na tunakubali matokeo lakini sitasahau alichokifanya refa, alikuwa na makosa mengi na maamuzi tata kibao ambayo yametugharimu kwa kiasi kikubwa.

“Sidhani kama marefa wa namna hii wataweza kulikomboa soka la Tanzania ambalo linataka kupiga hatua kutoka hapa lilipo kwa sababu hawajiamini na hata kuchezesha kwenyewe inakuwa shida na hata kusimamia maamuzi yao,” alisema Bossou.     


Katika mchezo huo, mwamuzi alikubali bao la pili la Mbeya City lakini baada ya kuzongwa na wachezaji wa Yanga waliodai haikuwa sahihi kwa kuwa faulo iliyopigwa ilitekelezwa bila ruhusa ya mwamuzi, refa huyo akaamuru faulo irudiwe, Mbeya City nao wakamzonga wakilalamika, akabadili maamuzi tena na kukubali kuwa ni bao na mpira uwekwe kati.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic