November 15, 2016



Kiungo wa Manchester City, Samir Nasri ambaye anakipiga Valencia kwa mkopo, amesema kocha Pep Guardiola aliwakataza kufanya ngono baada ya saa sita usiku.

Nasri ameliambia gazeti namba moja la michezo la L’equipe la Ufaransa kwamba, Guardiola aliwaambia baada ya saa sita usiku hakuna ngono kwa kuwa ni hatari kwao.

“Alisema ameweza kuwasaidia wachezaji kufanya vizuri kwa mfumo huo, alisema Messi au Lewandowski walifanya vizuri kutokana na kupunguza kufanya ngono baada ya saa sita.

“Alisema ukifanya hivyo unapata muda wa kutosha wa kupumzika na inasaidia sana,” alisema.

Nasri raia wa Ufaransa aliondoka Man City katika hatua za mwisho za kufunga dirisha baada ya kuona asingewezana na Mhispania huyo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic