November 2, 2016



Kila mwanadamu ataonja mauti, kila mwanadamu ana safari yake ya mwisho.

Safari ya mwisho ya bondia Thomas Mashali ilikuwa leo alipozikwa kwenye makabuli ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

Mashali alifariki dunia baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana.

Hadi anafariki dunia, Mashali alikuwa ni bondia namba mbili kwa viwango baada ya Francis Cheka lakini ikiwa ni miezi kadhaa baada ya kumtwanga Cheka.

Alikuwa na mikanda minne ya ubingwa katika mashirikisho mbalimbali likiwemo lile la UBO.


Mashabiki wengi walijitokeza leo kumuaga kwenye Viwanja vya Leaders kabla ya kumzika kwenye makaburi hayo ya Kinondoni.







0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic