ABBAS TARIMBA |
Mwenyekiti wa
zamani wa Yanga, Abbas Tarimba ameeleza majonzi yake kuhusiana na kifo cha
aliyekuwa makamu wake, Isaac Shekiondo.
Shekiondo aliyekuwa maarufu kama Clinton amefariki dunia leo katika Hospitali ya Amana
jijini Dar es Salaam.
Tarimba ambaye
alikuwa mwenyekiti na Clinton akiwa makamu, amesema alikuwa kiongozi shupavu na
mwenye utayari wa kujitolea.
“Mimi na akina
Shekiondo tulifanya kazi nzuri, nilimjulia Yanga lakini alijitoa na kujitolea,”
alisema.
“Katika masuala ya
kutofautiana na hoja, ilikuwa inatokea wakati mwingine tunapishana lakini lengo
lilikuwa ni kupata Yanga yenye matumaini na umoja.”
0 COMMENTS:
Post a Comment