November 21, 2016



Uongozi wa Yanga umeapa kutofanya papara katika suala la usajili na badala yake, kila kitu kitakwenda kiufundi.

Habari za ndani kutoka kamati ya mashindano ya Yanga zimeeleza, mambo yamekuwa yakifanyika taratibu na kufuata weledi.

“Hakutakuwa na chochote cha haraka, kila kitu kitakwenda kwa mpangilio na uongozi ndiyo unajua kila kitu. Lengo letu ni kufikia malengo.

“Hatuwezi kuwa na hofu kwa kuwa bado tuna kikosi bora, mabadiliko hayawezi kuwa makubwa kwa kuwa tunahitaji kuimarisha pekee,” kilieleza chanzo.

Imeelezwa, benchi la ufundi limeendelea kupewa nguvu ya kufanya mabadiliko ili mambo yakae sawa.


Yanga ndiyo timu inayoongoza kuwa na wachezaji wengi waliokaa pamoja na imeendelea kutesa kwa kutwaa ubingwa kwa misimu miwili mfululizo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic