January 20, 2017



Suluhu waliyoipata Azam, juzi Jumatano dhidi ya Mbeya City, imemfanya kipa wa Azam, Aishi Manula, kucheza mechi saba mfululizo ambazo ni sawa na dakika 630 bila ya kuruhusu wavu wake kutikiswa.

Manula ambaye anasifika kwa uhodari wa kuokoa mikwaju ya penalti, amefanikiwa kufanya hivyo katika michezo miwili ya Ligi Kuu Bara na Kombe la Mapinduzi.

Mara ya mwisho kwake kuruhusu bao ilikuwa ni Desemba 24, mwaka jana kwenye sare ya bao 1-1 dhidi ya Majimaji kwenye Uwanja wa Majimaji, Songea.

Baada ya hapo, akaiongoza Azam kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Prisons, kisha kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi matokeo yalikuwa hivi; Azam 1-0 Zimamoto, Azam 0-0 Jamhuri, Azam 4-0 Yanga, Azam 1-0 Taifa Jang'ombe na Azam 1-0 Simba.

Manula anatakiwa kufanya hivyo kwenye mechi nne zijazo ili kuipiku rekodi ya Muivory Coast, Vincent Angban ambaye kabla ya kuvunjiwa mkataba na Simba, msimu huu alicheza mechi kumi za kimashindano bila ya kuruhusu bao.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic