February 23, 2017


MAJIMAJI

Kikao cha Bodi ya Kusimamia na Kuendesha Ligi, kiliketi mwanzoni mwa wiki hii na kufanya tathmini ya mambo mbalimbali yaliyotokea kwenye michezo mbalimbali ya mpira wa miguu kwa michuano yote – Ligi Kuu ya Vodacom, Ligi Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili.

Haya haya ndiyo yaliyojiti katika kila mchezo.

Mechi namba 170 (Stand United FC vs Majimaji). Majimaji iliwasilisha malalamiko kuwa chumba chao kubadilishia nguo (changing room) kilipuliziwa na timu pinzani dawa ambayo ni sumu, hivyo kushindwa kukitumia wakati wa mapumziko.


Klabu ya Stand United FC pamoja na Meneja wa Uwanja waandikiwe barua kuwa vitendo hivyo vikiendelea kujitokeza uwanja huo utafungiwa kwa mechi za Ligi Kuu ya Vodacom.



Msimamizi wa Kituo aandikie taarifa yake (report) kuhusu tukio hilo. Pia Daktari wa Uwanja, Dk. Abel Kimuntu awasilishe taarifa yake ya kitaalamu kuhusu suala hilo, vilevile Meneja wa Uwanja huo, Meja mstaafu Mohamed Ndaro naye awasilishe taarifa yake kuhusu tuhuma hizo za kumwaga dawa kwenye vyumba.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic