Kikosi cha timu ya taifa ya Burundi, tayari kipo nchini kwa ajili ya mechi ya kirafiki dhidi ya Taifa Stars, Jumanne.
Mshambuliaji wa Simba, Laudit Mavugo ameungana na kikosi hicho leo.
Lakini Amissi Tambwe, yeye ni majeruhi, hakuitwa katika kikosi hicho.
Mavugo atacheza dhidi ya Stars Jumanne, huku akitarajiwa kuchuana na beki wa Simba, Abdi Banda ambaye wanacheza kikosi kimoja, kama Kocha Salum Mayanga atampanga.
0 COMMENTS:
Post a Comment