August 17, 2017


Kiungo Mbrazil, Paulinho ameamua kuondoka China na kutua Barcelona kwa day la pauni million 36.5.

Paulinho alikuwa akikipiga Guangzhou Evergrande inayoshiriki China Super League.


Tayari amekabidhiwa jezi namba 15 Camp Nou na Barcelona inaonekana imepania kuongeza nguvu katika kikosi chake kinachoonekana kutokuwa vizuri kama wanavyotaka kabla ya kuanza La Liga.

Pamoja na kukabidhiwa jezi, Paulinho alikabidhiwa zawadi ya gari jipya aina ya Audi A7. Kampuni ya Audi ni wadhamini wa Barcelona.







0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic