September 22, 2017




Aliyekuwa Kocha Mkuu wa Njombe Mji, Hassan Banyai amezitaja sababu mbili zilizomfanya aamue kuachana na timu hiyo.

Banyai amesema sababu ya kwanza ni kutishiwa maisha na watu waliokuwa wanamuambia aawaachie timu yao.

“Lakini kulikuwa na viongozi pia wanaingilia kazi zangu, unapanga kikosi hiki, wao wanakuja wanalazimisha mchezaji fulani lazima acheze.

“Hakukuwa na utaratibu mzuri na kuheshimu taaluma, badala yake kila mtu anajua ukocha,” alisema.


Uongozi wa Njombe Mji, ulipokea barua yake ya kujiuzulu na kumtakia kila la kheri na sasa aliyekuwa msaidizi wake, Mrage Kabange ndiye anayeshikilia nafasi hiyo. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic