October 20, 2017



Kocha Mkuu wa Yanga, George Lwandamina amefunguka kuwa hakuna pengo lolote ndani ya kikosi chake licha ya kuwakosa baadhi ya wachezaji nyota wa timu hiyo, Thabani Kamusoko na Donald Ngoma ambao ni majeruhi.

Kocha huyo amesema hayo wakati wachezaji hao Jumamosi iliyopita walishindwa kuwa sehemu ya kikosi cha Yanga ambacho kilishuka dimbani kumenyana na Kagera Sugar ambao walishinda kwa mabao 2-1, kwenye mchezo wa ligi kuu uliopigwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Kamusoko yuko nje akisumbuliwa na kifundo cha mguu (enka) ambapo atazikosa mechi zote za timu hiyo Kanda ya Ziwa dhidi ya Kagera Sugar na Stand United, huku Ngoma akisumbuliwa na majeraha ya goti.

Lwandamina amesema kwake haoni shida ya kutokuwa na wachezaji hao kwenye kikosi hicho kutokana na uwepo wa wachezaji wengine ambao wanaifanya kazi vizuri na kupata matokeo.

“Huwezi kusema kwamba kuna pengo la Ngoma au Kamusoko kwa sababu unapozungumzia timu ni juu ya watu wote ambao wapo na hali ya umoja iliyopo na siyo suala la mchezaji mmoja pekee, ndiyo maana utaona hatukuwa nao lakini tumepata matokeo mazuri.

“Kwangu hakuna pengo la mchezaji yeyote yule kutokana na waliopo kuifanya kazi vizuri na matokeo tunapata, kuna zaidi ya wachezaji 20 hapa sasa wanapokosekana wachezaji wawili au watatu hilo siyo pigo hata kidogo kwetu, kwani ninachukua mbadala wake na ninamtumia,” alisema kocha huyo wa zamani wa Zesco United ya Zambia.

SOURCE: CHAMPIONI


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic