Kikosi cha Simba kimetua mjini Zanzibar na kuanza kambi yake rasmi kuiwinda Yanga.
Simba inajiandaa katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Yanga kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Wachezaji wa Simba chini ya Kocha Joseph Omog, wamepanga kuanza mazoezi magumu kesho asubuhi na watafanya mazoezi asubuhi na jioni kwa siku mbili mfululizo.
Mechi hiyo inasubiriwa kwa hamu kutokana na Simba na Yanga kulingana pointi, kila moja ikiwa na 15 na Simba ikiwa kileleni kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment