November 18, 2017


Mrembo wa zamani wa taji la Miss Chang’ombe na mwigizaji maarufu nchini, Irene Uwoya amewasili jijini Kigali, Rwanda kuhani msiba wa aliyekuwa mumewe, Ndikumana Hamad.

Ndikumana aliyekuwa akijulikana kama Katatut, alifariki dunia ghafla siku chache zilizopita na kuzikwa juzi jijini Kigali.

Uwoya hakuwa jijini Kigali wakati wa mazishi na usiku wa kuamkia leo ametua jijini Kigali akiongozana na mwanaye, Klishy ambaye alizaa na marehemu. Pia aliongozana na mama yake mzazi.

Uwoya alijifunika sura muda wote wakati akiwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kanombe jijini Kigali.



Wakati anatua, ndugu wakiwemo mashabiki wa michezo na burudani, walijitokeza uwanjani hapo.

Kataut ambaye alicheza soka katika nchi kadhaa za Ulaya, mauti yalimkuta akiwa kocha msaidizi wa Rayon Sports na siku moja kabla ya kifo chake alikuwa mazoezini.

Kwa hapa nchini, Kataut aliwahi kuichezea Stand United kabla ya Kocha Patrick Liewig raia wa Ufaransa, kupendekeza aachwe.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic