November 22, 2017




Hatimaye mshambuliaji nyota wa Yanga, Amissi Tambwe ameanza mazoezi na wenzake.

Tambwe ambaye hajacheza hata mechi moja ya Ligi Kuu Bara msimu huu, leo ameanza mazoezi na wenzake wakati Yanga ikijifua kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.

Awali, kwa takribani siku nne, Tambwe amekuwa akizunguka uwanja peke yake wakati wenzake wakiendelea na mazoezi.

Lakini leo amejumuika na wenzake katika mazoezi na ameonyesha kuwa yuko vizuri kutokana na kushiriki katika zoezi la upigaji mashuti.

Tambwe amekuwa kati ya wachezaji waliopiga mashuti makali katika mazoezi ya leo.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic