December 11, 2017


Kocha Msaidizi wa Simba, Mrundi, Masoud Djuma, amesema kuwa, kwa muda mchache aliokuwa akimfanyia majaribio straika Mzambia, Jonas Sakuwaha, amemuona anafaa kusajiliwa kikosini hapo, hivyo kilichobaki kamati kufanya kazi yake.

Mzambia huyo ambaye alianza majaraibio wiki mbili zilizopita, Ijumaa iliyopita alifunga bao moja katika ushindi wa 3-1 walioupata dhidi ya KMC katika mchezo wa kirafiki uliopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar.

Akizungumzia uwezo wa mchezaji huyo, Masoud alisema: “Kabla ya hapo sikuwahi kumuona, lakini nilipokabidhiwa ndiyo nikaanza kuuona uwezo wake.

“Nilikuwa nampeleka uwanjani kufanya mazoezi wakati timu ilipokuwa mapumzikoni, alianza taratibu lakini kila siku zilivyokuwa zinakwenda akawa anazidi kuwa vizuri.

“Inaonyesha anaipenda sana kazi yake na hicho ndicho kimemsaidia mpaka nikamuona anatufaa. Ni mzuri katika kujiweka kwenye nafasi kutokana na nafasi anayocheza, ni nadra kwake kupoteza mpira akiwa nao, lakini pia ni msumbufu kwa mabeki. Sasa mchezaji kama huyo ndiyo anahitajika.

“Mimi kazi yangu ilikuwa ni kumuangalia uwezo wake na nimeridhika naye, hivyo naiachia kamati ifanye kazi yake, kwa upande wangu hana shida yoyote, akisajiliwa atatusaidia.

Endapo Mzambia huyo atasajiliwa, ina maana kwamba Simba itatakiwa kupunguza mchezaji mmoja wa kimataifa kwani hivi sasa wapo saba.


Alipoulizwa Mrundiu huyo ni nani atapunguzwa ili Mzambia huyo asajiliwe, alisema: “Hiyo siyo kazi yangu, uongozi ndiyo unajua, lakini mpaka usajili utakapofungwa atajulikana ni nani tunamuacha kwa sababu mchezaji kuhama timu ni kawaida.”

1 COMMENTS:

  1. TUNAJIDANGANYA::---
    Kocha lazima ajue ni nani anayetakiwa kuachwa na si Uongozi. Uongozi unapitia mapendekezo ya benchi la ufundi. Mi naamini yupo mchezaji ambae ameshapendekezwa na benchi la ufundi katika dirisha dogo aachwe ili apatikane mwingine.

    Siwezi amini kuwa Djuma hajui ni nani wa kumuacha kwa kuwa yeye ndio mtoa taarifa akimsaidia Omog. Hawa ndio mwisho wanasema Uongozi unatuingilia majukumu wakati yeye mwenyewe ndio anasema hajui ni nani wa kumuacha.

    Kingine...tusisajili ili kuonekana mbele ya macho ya watu kuwa tunataka kusajili..ndio tutabaki palepale kuwa hatuwezi kupata mchezaji ambae yupo vizuri katika nchi zilizotutangulia hadi pale awe ameshamaliza kucheza mpira wa ushindani. Inavyosemekana..mchezaji huyu keshacheza TP Mazembe..sijui ya kipindi gani...kacheza pale Sudan..na sehemu zingine. Mwisho anakuja huku Tanzania. Je wewe unaona Bilioni ya Mo itafanya kazi inavyotakiwa kwa kuwachukua wachezaji "mechi moja anacheza na mechi ya pili majeruhi"??embu tumuonelee huruma muwekezaji wetu.

    Tutafute vijana hata kama ni wawili lakini wenye Uwezo mkubwa.Kama hela ipo kwanini uchukue magari mabovu. Twende Afrika Kusini weka mezani pesa Chuku hawa watu pale Orlando Pirates...(Thabo Rakhale and Thabo Qalinge, Thempo Matete na Zongo). Tumia hela upate wachezaji hawa..naamini ukimchukia Thaboa Rakhale hata Niyonzima huwezi taka kumuona uwanjani

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic