February 18, 2013




Wapi anakoelekea Arsene Wenger kutoka alipo sasa? Inaonekana kama mashabiki wa Arsenal nchini England wanaweza kuacha kuingia kwenye Uwanja wa Emirates.
Kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Blackburn Rovers maana yake timu hiyo haina nafasi ya kubeba kwa miaka nane mfululizo sasa. Inaonyesha wana Arsenal kweli wamechoka.
Mwaka 2009, Emmanuel Adebayor alijiunga Man City ada ya pauni milioni 25, nafasi yake ikazibwa na Marouane Chamakh miezi 10 baadaye, kwa uhamisho usiokuwa na malipo kutoka Bordeaux ya Ufaransa.
William Gallas akatua Tottenham bila malipo, siku nne baadaye Sebastien Squillaci kutoka Sevilla akatua Arsenal.
Mwisho wa msimu wa 2010, Cesc Fabregas, Samir Nasri na Gael Clichy wakauzwa na nafasi zao zikazibwa na Mikel Arteta, Gervinho na Andre Santos.
Msimu huu, Robin van Persie kauzwa Man United kwa pauni 22m, halafu Wenger akamnunia Olivier Giroud kutoka Montpellier ya Ufaransa kwa pauni 3m.
Kwa wote wapya, angalau kidogo Arteta ameonyesha mafanikio, tena si kwa kiwango cha juu sana.
Lakini Giroud pia kajitahidi, wengine wote bado ni angalau tu, mfano; Santi Cazorla, Lukas Podolski, Thomas Vermaelen, Alex Oxlade-Chamberlain na Per Mertesacker ni wazuri lakini bado hawajaonyesha Arsenal imeweza kutibu ugonjwa wake.
Kinachoonekana hapa Wenger anapoteza wachezaji wa kiwango cha juu zaidi halafu anachukua wale wa bei nafuu na kuwatengeneza.
Uongozi hauna tatizo naye, hakuna makombe lakini faida inaingia kubwa. Mashabiki hawataki kuelewa hadithi za faida bila ya makombe.
 Ndiyo maana wengi wanaingia katika mjadala, inaonekana Wenger ndiye adui wa watu wote hasa mashabiki wa Arsenal.
Ila kichekesho, wakati mashabiki wanataka aondoke, uongozi unaonyesha tayari kumuongezea mkataba wa miaka miwili. KAZI IPO.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic