March 19, 2015


Pamoja na kuwa na Simon Msuva na Mrisho Ngassa, Kocha Hans van der Pluijm ameutaka uongozi wa Yanga kuongeza kiungo wa pembeni mwenye kasi.


Pluijm raia wa Uholanzi ameueleza uongozi wa Yanga kuwa anataka kiungo mwenye kasi kwa ajili ya kuimarisha kikosi.

“Kocha ametaka kuongezewa kiungo mwingine mwenye kasi. Suala hilo amelifikisha kwa uongozi naye ameambiwa apendekeze.

“Kati ya wachezaji aliowapendekeza ni kiungo mmoja wa zamani wa Simba. Sasa suala linafanyiwa kazi.
“Pia tunaangalia sehemu mbalimbali, lengo ni kuboresha zaidi kikosi,” kilieleza chanzo cha uhakika.


Kuhusiana na suala la usajili, Pluijm amekuwa akisisitiza kwamba si wakati wa kuzungumzia kwa madai ni mapema mno.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic