July 6, 2016


Uongozi wa Azam FC umeamua hasa, baada ya kumshusha kipa kutoka Tenerife ya Hispania, sasa kuna kipa wa timu ya taifa ya Ivory Coast.

Huyu ni Daniel Yeboah Tetchi ambaye yuko jijini Dar es Salaam tayari kumalizana na Azam FC ili aitumikie msimu ujao.

Kipa huyo mwenye umri wa miaka 31, alianza kuonyesha cheche zake akiwa Asec Mimosa ya Ivory Coast.
Pia amewahi kuitumikia Dijon ya Ufaransa katika kikosi chake cha pili.


Habari za uhakika zinaeleza, Tetchi yuko katika nafasi kubwa ya kumalizana na Azam FC lakini suala la kipa Mhispania linaweza kuweka ushindani mbele yake.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic