January 23, 2017


Kocha mpya wa Azam FC, Mromania, Aristica Cioaba, kwa mara ya kwanza Jumamosi ijayo anatarajiwa kukaa katika benchi kuiongoza timu hiyo itakapopambana na Simba kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa Uwanja wa Uhuru, Dar.

Mromania huyo ambaye amepewa mkataba wa miezi sita na Azam akichukua nafasi ya Mhispania, Zeben Hernandez aliyetimuliwa mwishoni mwa mwaka jana, bado hajaanza kazi rasmi ya kuinoa timu hiyo kutokana na kukosa kibali cha kufanyia kazi hapa nchini.

Meneja wa timu hiyo, Philip Alando, amesema: “Kila kitu tumekamilisha kwa maana ya kulipia gharama za kupata kibali, kilichobaki kwa sasa ni kusubiri tu uhamiaji kuona ni lini watatupatia hicho kibali.

“Kwanza tumeomba kibali cha kazi, tutakapokipata, ndipo tutafanya mchakato wa kuomba kibali cha makazi, matarajio yetu ni kuona kabla hatujapambana na Simba tumekamilisha kila kitu ili kocha wetu huyu aanze rasmi kazi.”


Ikumbukwe kuwa, kwa sasa kikosi cha Azam kinanolewa na kocha wa muda, Idd Nassor Cheche baada ya Zeben na benchi lake la ufundi lililokuwa likiundwa na Wahispania watano kufutwa kazi kutokana na matokeo mabaya waliyokuwa wakiyapata.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic