January 25, 2017



Mwamuzi wa mchezo wa hatua ya awali wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Yanga na Ngaya Club DE Mbe ya Comoro, amewekwa hadharani na Shirikisho la Soka Afrika (Caf).

Mchezo huo unaotarajiwa kupigwa Februari 12, mwaka huu kwenye Uwanja wa Stade de Moroni uliopo katika Mji wa Moroni nchini Comoro, utachezeshwa na mwamuzi wa kati raia wa Shelisheli, James Fedrick Emile.


Caf ikiwa tayari imemtaja mwamuzi huyo wa kati, lakini bado haijawaorodhesha wasaidizi wake ambao ni washika vibendera wawili, mwamuzi wa mezani na msimamizi wa mchezo huo.


Baada ya mchezo huo, timu hizo zitarudiana Februari 17, mwaka huu jijini Dar na mshindi wa jumla atacheza hatua ya pili dhidi ya Zanaco ya Zambia au APR ya Rwanda.



Yanga ambao ni wawakilishi wa Tanzania Bara kwenye michuano hiyo, kwa sasa inaendelea na maandalizi makali kuhakikisha inafanya vizuri huku ikiwa tayari imeanza harakati za chini chini za kuwachunguza wapinzani wao hao.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic