Kocha wa makipa wa Yanga, Juma Pondamali 'Mensah' ameonyesha yuko fiti baada ya kumbeba kiungo Haruna Niyonzima raia wa Rwanda.
Pondamali alimruhusu Niyonzima kuukwea mgongo wake, yeye akaonyesha yuko fiti kwa kuendelea kutembea huku akisisitiza, wala hajateteleka.
Wawili hao walikuwa wakitania wakati wa mazoezi ya Mabingwa hao wa Ligi Kuu Bara na Mabingwa wa Kombe la Shirikisho. Mazoezi hayo yalifanyika kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, leo.
0 COMMENTS:
Post a Comment