Mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga wanaendelea namazoezi yao asubuhi hii.
Yanga ambao wikiendi hii itashuka uwanjani Jumapili kuwavaa Mwadui FC kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.
Kocha George Lwandamina amesema leo asubuhi wanaendelea na mazoezi kama kaiwaida.
“Tunaendelea na maandalizi ya michezo ijayo ya ligi. Sasa tunalenga zaidi Mwadui,” alisema.
Yanga iko katika nafasi ya pili ikiwa na pointi 43 nyuma ya Simba yenye pointi 45 kileleni.
0 COMMENTS:
Post a Comment