Kumekuwa na mjadala unatembea mitandaoni kuhusiana na Haji Manara kuangua kilio mahakamani Kisutu, jana.
Manara ambaye ni msemaji wa Simba, aliangua kilio baada ya Rais wa Simba, Evans Aveva na makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kutakiwa kwenda mahabusu baada ya kusomewa mashitaka ya utakatishaji fedha.
Suala hilo lilionyesha kumuumiza Manara ambaye alitafuta sehemu akakaa na kuangua kilio hasa baada ya kusikia wanakwenda mahabusu hadi Julai 13, kesi yao itakaposikilizwa leo.
Katika makundi mbalimbali ya Whatsapp ambayo yanahusisha Yanga au Simba, wengi wamekuwa wakimuonea huruma Manara kutokana na picha zinazomuonyesha akiangua kilio.
Kinachomliza nini? Hajui takukuru wanasimamia maslahi ya Simba? Au naye anahusika? Atulie tu haki ifuate mkondo wake. Kama hawahusiki si watatoka? Unaweza lia halafu mwishoni ikathibitika walifanya ufisadi, tutakuweka kundi gani? Labda kama analilia rafiki zake tu
ReplyDeleteKinachomliza nini? Hajui takukuru wanasimamia maslahi ya Simba? Au naye anahusika? Atulie tu haki ifuate mkondo wake. Kama hawahusiki si watatoka? Unaweza lia halafu mwishoni ikathibitika walifanya ufisadi, tutakuweka kundi gani? Labda kama analilia rafiki zake tu
ReplyDelete