June 30, 2017





Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amesema alihojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Hans Poppe amesema alihojiwa lakini akaachiwa na si anashikiliwa kama ambavyo imekuwa ikielezwa.

“Nilikwenda, nikahojiwa na baadaye nimeondoka, niko mitaani. Si kweli kwamba ninashikiliwa.

“Kuhusiana na kuhojiwa tayari nilihojiwa kama mara mbili hivi kabla. Haya ni mambo yanatokea,” alisema Hans Poppe.


Jana kulikuwa na taarifa kwamba Hans Poppe naye alikuwa anashikiliwa na Takukuru baada ya Rais wa Simba, Evans Aveva na Makamu wake, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ kupandishwa kizimbani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic