Aliyekuwa kocha msaidizi wa timu ya Simba, Masoud Djuma ambaye aliwasili nchini October 2017 akichukua nafasi ya Jose Mayanja, amepata shavu la kuinoa timu ya As Kigali inayoshiriki ligi kuu nchini Rwanda.
Djuma alikuwa kocha msaidizi Msimbazi, anakuwa kocha mkuu ndani ya timu mpya ambayo amesaini kandarasi ya mwaka mmoja mara baada kocha mkuu wa timu hiyo Eric Nshimiyimana kujiuzulu.
Timu nyingine ambayo ilikuwa ikihitaji saini ya Djuma baada ya kuachana na Simba kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutokuwa na maelewano mazuri na kocha mkuu wa Simba Patrick Aussems ni Inter Class ya Burundi ambayo inashiriki ligi daraja la pili.
0 COMMENTS:
Post a Comment