BOCCO AITAJA KAZI KUBWA WALIYONAYO SIMBA
Nahodha wa Simba, John Bocco amesema kuwa, wana kazi kubwa ya kufanya ili kuibuka na ushindi katika mchezo wa leo Jumamosi dhidi ya Nkana FC kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika lakini lazima washinde.
Simba itacheza na Nkana ukiwa ni mchezo wa kwanza utakaochezwa nchini Zambia wa Hatua ya Kwanza ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Simba ambayo iliondoka Jumatano ya wiki hii kwenda kucheza mchezo huo, inaisaka nafasi ya kutinga makundi ya michuano hiyo mikubwa Afrika kwa ngazi ya klabu.
“Tuna kazi kubwa ya kufanya mbele ya Nkana ili tuweze kuvuka hatua hii ambayo kila mmoja wetu hapa anatamani kuona tunatinga makundi.
“Suala la kwanza hapa ni kushinda na si kitu kingine, hatufikirii matokeo mengine tofauti, tunataka kufikia malengo yetu na ndiyo maana tunahitaji kushinda,” alisema Bocco.
Ikumbukwe kuwa, baada ya mchezo huo, timu hizo zinatarajiwa kurudiana Desemba 23, mwaka huu jijini Dar ambapo mshindi wa jumla atacheza hatua ya Makundi. Atakayefungwa, ataenda kucheza mechi za mtoano kuwania kucheza hatua ya Makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika
Komaaeni hatuna timu ya taifa zaidi ya simba tuna wategemeeni ili kuiwakirisha Tanzania yetu vizuri
ReplyDeleteMungu ni mkubwa atakuwa pamoja nanyi kwa uwezo wake
ReplyDeleteNaamin MUNGU atatusaidia timu yetu ya simba kushinda
ReplyDeleteKila LA heri SSC, naamini mtatutoa kimasomaso, tutawatoa tu hao jamaa pamoja na kuwa walishatutoa awamu 2 kwa ziada ya goli 1. Awamu hii ni wetu mungu awape moyo na ujasiri wa kupambana ugenini na kupata ushindi au walau droo ili mechi ya 2 tuwachinjie pale taifa. Jamaa inaonesha huwa wanategemea sana uwanja wao kwani ugenini hawana chochote. So in kuwamaliza mapema hukohuko kwao. Aminia sana SSC, Kila LA kheri.
ReplyDeleteKila la kheri timu yetu ya simba
ReplyDelete