August 22, 2019



UONGOZI wa Azam FC umesema kuwa kuelekea kwenye mchezo wa marudio dhidi ya Fasil Kenema ya Ethiopia umejipanga kulipa kisasi ukiwa nyumbani Jumamosi ya wiki hii Uwanja wa Chamazi.

Azam FC mchezo wa awali nchini Ethiopia ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0, kwa sasa inahitaji ushindi kwenye mchezo wa marudio ili kusonga mbele ili wakutane na mshindi wa mchezo kati ya Triangle FC ya Zimbabwe ama Rukinzo ya Burundi na itaanzia nyumbani kati ya Septemba 13-15.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Azam FC, Jaffary Maganga  amesema kuwa kikosi kimeanza maandalizi kwa ajili ya mchezo huo.

“Tayari Kocha Ettienne Ndayiragije ameanza kuwapa program maalumu vijana kwa ajili  ya kupata matokeo chanya kwenye mchezo wetu wa marudio tuna imani ya kufanya vizuri kwani tutakuwa nyumbani.

“Uwanja wa Chamazi hakuna kinachoshindikana kwani wachezaji wanautambua vema uwanja na morali ya kusonga mbele kwenye michuano hii mikubwa Afrika upo juu, mashabiki wajitokeze kwa wingi,” amesema.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic