KOCHA Mkuu wa
Biashara United, Amri Said amesema kuwa kikosi kipo tayari kawa ajili ya mchezo wa dhidi ya Kagera Sugar utakaochezwa Agosti 24 uwanja wa Karume.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Said amesema wamejiandaa kutoa burudani kwa mashabiki
na kuleta ushindani wa kweli.
“Tunatambua
mchezo utakuwa mgumu ila lazima tupambane kupata matokeo, wachezaji wana morali na wanajua mchezo hautakuwa mwepesi,” amesema.
Msimu
uliopita wa mwaka 2018/19 walipokutana uwanja wa Karume matokeo ilikuwa 0-0.
0 COMMENTS:
Post a Comment