PATRICK Aussems, Kocha Mkuu wa Simba amesema kuwa ana imani na kikosi chake kitapata
ushindi mbele ya wapinzani wao UD do Songo kwenye mchezo wa marudio
utakaochezwa Agosti 25 uwanja wa Taifa.
Simba ililazimisha suluhu ya bila kufungana kwenye mchezo wa awali wa Ligi ya
Mabingwa uliochezwa uwanja wa Beira, nchini Msumbiji.
Akizungumza
na Saleh Jembe, Aussems amesema ana imani kubwa na kikosi chake kupata ushindi kwenye mchezo wa marudio.
“Kikubwa ninachoshukuru ni kwamba hatujaruhusu bao tulipkuwa ugenini sasa kazi yetu imebaki kutafuta ushindi mbele ya wapinzani wetu.
“Ambacho kinanipa matumaini ni nguvu ya mashabiki wa Simba pamoja na uzuri wa
uwanja wa nyumbani, hakuna namna nyingine tutakayofanya zaidi ya kutafuta
matokeo.” Amesema Aussems.
Ujumbe umefika nasi tutaujaza uwanja kutetea heshima ya Tanzania na Simba yenyewe na tunamuomba Mungu awe nasi pamoja timu zote za nyumbani zinazoshiriki mechi hizi za kitaifa
ReplyDeleteAmiin
ReplyDeleteAmiin
ReplyDelete