February 21, 2020


BAKARI Mwamnyeto, nahodha wa Coastal Union amesema kuwa watapambana mbele ya Yanga kupata matokeo chanya kwenye mchezo wa kesho utakaopigwa Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.

Coastal Union iliyo chini ya Juma Mgunda inakumbukumbu ya kufungwa mchezo wa kwanza na Yanga Uwanja wa Uhuru bao 1-0.

"Kikubwa ni maandalizi na kupoteza mchezo wetu uliopita inaumiza ila matokeo ya mpira yapo namna hiyo wapinzani wanapambana nasi ni lazima tupambane, mashabiki watupe sapoti," amesema. 

Coastal Union ilifungwa mabao 2-1 na Ruvu Shooting kwenye mchezo wao wa ligi ulipita itamenyana na Yanga iliyopata sare ya kufungana bao 1-1 na Polisi, Tanzania Februari 23.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic