February 21, 2020

PAPY Tshishimbi, nahodha wa Yanga amesema kuwa matokeo yao ya sare wanayopata uongozi utafanyia kazi makosa yao.

Februari 23 Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Yanga itamenyana na Coastal Union kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara ikiwa na kumbukumbu ya kulazimisha sare mchezo wao uliopita mbele ya Polisi Tanzania kwa kufungana bao 1-1.

"Sare ambayo tumepata ni mbaya sasa hapo Kocha Mkuu yeye anajua wapi tulikosea na namna gani tufanye ili kupata matokeo kwenye mechi zetu zijazo. Tunapambana kupata matokeo mazuri mashabiki watupe sapoti," amesema.

Yanga imepata sare tatu mfululizo sawa na dakika 270 ilianza mbele ya Mbeya City kwa kufungana bao 1-1 kisha Tanzania Prisons sare tasa na kwenye mcheo wao uliopita dhidi ya Polisi Tanzania ilikuwa ni 1-1. 

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic